728x90 AdSpace

Latest News

Wednesday, October 1, 2014

Mh. Lowassa amkaribisha Monduli Balozi wa Japan nchini Tanzania


Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akimkaribisha wilayani Monduli Balozi wa Japan nchini Tanzania,Mh. Masaki Okada wakati alipowasili wilayani humo jana Jumapili Septemba 28,2014 kwa ajili ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayofadhiliwa na nchi hiyo.Balozi huyo aliahidi kusaidia vifaa vya kisasa katika hospitali mpya ya kisasa inayojengwa wilayani humo.Meneja wa Hoteli ya Emanyata mjini Monduli,Bi. Neema (kushoto) akimkaribisha Balozi wa Japan nchini Tanzania,Mh. Masaki Okada hotelini hapo.Pembeni kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Monduli,Bw. Twalib Mbasha. Balozi wa Japan nchini,Mh. Masaki Okada (katikati) akiwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli,Twalib Mbasha (kulia) na Meneja wa Hoteli ya Emanyata mjini Monduli,Bi. Neema alikofikia balozi huyo na ujumbe wake katika ziara yake ya siku mbili wilayani humo.
Michuzi
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: Mh. Lowassa amkaribisha Monduli Balozi wa Japan nchini Tanzania Description: Rating: 5 Reviewed By: Unknown
Scroll to Top